AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Ndugu Ahmed Albaity ambaye amekuwa akisumbuliwa na tatizo la uti wa mgongo ambalo limedumu kwa takribani miaka kumi na moja akiwa kitandani,tayari ameanza kupatiwa Matibabu katika hatua za awali mara tu baada ya kuwasili hospitalini hapo.
Mapema akizungumza kwa niaba ya Wanafunzi wakitanzania Wanaosoma na kuishi nchini humo Bw. Remidius Emmanuel ambaye pia ni Katibu Mkuu Shirikisho hilo amesema wao kama watanzania wanaosoma na kuishi katika Taifa la China wameshiriki kumpokea Mtanzania mwenzao (Ndugu. Ahmed Albaity ) na kwamba kwa kipindi chote ambacho atakuwepo hapa Beijing China wataendelea kutoa Ushirikiano na kumjulia hali wakati wote.
"Tunamshukuru Mwenyezi MUNGU amemuongoza Bw.Ahmed kufika salama hapa Beijing, Tumeshuhudia watanzania wakimsindikiza uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe.Paul Makonda, huu ni upendo wa kipekee, na sisi tumeguswa na kuwiwa kumpokea tukiongozwa na Maafisa waandamizi wa Ubalozi wetu hapa China" Alisema Bw. Remidius.
Kwa upande wake ndugu Ahmed Albaity ameushukuru Ubalozi wa Tanzania nchini China pamoja na uwakilishi wa Watanzania wanaosoma na kuishi nchini humo kwa moyo wao wa upendo na namna walivyoweza kumpokea yeye na ujumbe alioambatana nao.
Bw.Michael Semindu moja kati watanzania wanaosoma nchini humo aliyeshiriki mapokezi hayo alimhakikishia Ndugu Ahmed Ushirikiano kwa kipindi chote atakachokuwa kwenye matibabu jijini Beijing "Nimefurahi kuungana na Maafisa wa Ubalozi pamoja na watanzania wenzangu kumpokea mwenzetu, tunamuahidi ushirikiano kwa kipindi chote atakachoendelea kupata matibabu nchini China" Alisema Bw. Michael
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK