AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Neymar mwenye umri wa miaka 26, atasafirishwa hadi Brazili wiki hii kwaajili ya matibabu huku madaktari kutoka ndani ya klabu ya PSG na timu yake ya taifa ya Brazili wakishirikiana pamoja kuhakikisha mshambuliaji huyo ghali zaidi duniani anarejea katika hali yake ya kawaida.
Taarifa iliyothibitishwa na klabu ya Paris Saint-Germain ya nchini Ufaransa hapo jana siku ya Jumatano ni kuwa mshambuliaji huyo ataukosa mchezo wa marudiano wa klabu bingwa barani Ulaya dhidi Real Madrid.
Baada ya matibabu ya siku tatu yaliyo waunganisha madaktari wa pande zote mbili klabu ya Paris Saint-Germain na timu ya taifa ya Brazil mchezaji mwenyewe Neymar Jr amependekeza kutibiwa nchini kwao mwishoni mwa wiki hii.
Atakuwa chini ya Dr. Rodrigo Lasmar kwa upande wa Brazili na Profesa Saillant atakayeiwakilisha PSG.
Meneja wa PSG, Unai Emery hapo hawali alisema kuna uwezekano mdogo kwa Neymar kuwepo katika mchezo ujao wa klabu bingwa siku ya Jumanne dhidi ya Real Madrid.
PSG, itakosa huduma ya Neymar dhidi ya mwenye jumla ya mabao 19 na pasi 13 zilizochangia mabao msimu huu Ligue 1.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK