Idadi ya Waliofariki Katika Ajari Mkoani Tabora Yaongezeka

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Idadi ya Waliofariki Katika Ajari Mkoani Tabora Yaongezeka
Idadi ya watu waliofariki kwenye ajali ya basi mkoani Kagera imeongezeka na kufikia saba, ambapo wengine wawili walifariki wakiwa hospitali.

Akizungumza na www.eatv.tv, Kamanda wa Polisi mkoa wa Kagera Agustino Olomi amesema mpaka jana jioni ilivyotokea ajali watu watano ndio walikuwa wamefariki, lakini mpaka sasa wengine wawili wameongezeka na kufanya idadi kufikia saba.

Ajali hiyo imetokea katika kijiji cha Kasharazi wilayani Ngara mkoani Kagera, ambapo moja ya basi kati ya mabasi manane yaliyokuwa yamebeba wakimbizi yakiwa kwenye msafara sambamba na magari mengine madogo, kufeli breki na kugonga basi lingine, na kusababisha kumgonga muendesha baiskeli na kufariki papo hapo, kisha basi hilo kupinduka na kusababisha vifo vya watu wanne hapo hapo.

Kamando Olomi amesema mpaka sasa hawajajua idadi ya majeruhi kwani wakimbizi hao ambao walikuwa wakitokea kwenye kambi ya Nduta Wilayani Kibondo mkoani Kigoma na kuelekea Burundi, kupelekwa kwenye kambi ya wakimbizi karibu na eneo hilo, na wahusika wa kambi ndio wanahusika na taarifa zao.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad