Johari Afunguka Kuhusu Kushindwa Kumtembelea Lulu Gerezani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Johari Afunguka Kuhusu Kushindwa Kumtembelea Lulu Gerezani
Msanii nguli wa filamu Tanzania Blandina Chagula alimaarufu kama Johari amefunguka na kuweka wazi sababu kubwa inayomfanya ashindwe kwenda kumtembelea msanii mwenzake wa filamu Lulu Michael gerezani.


Johari akiwa kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV kila siku ya Jumatano kuanzia saa nane mchana amesema kuwa toka Elizabeth Michael amefungwa hajawezi kwenda gerezani kumtembelea na kumjulia hali kwa kuwa anahofia kwenda kwake ni kuzidi kumuongezea uchungu na upekwe.

"Kiukweli toka Lulu amefungwa jela sijawahi kwenda kumsalimia, kwa upande wangu naona unapokwenda kutembelea ni sawa na kumuongezea machungu na upekwe zaidi hivyo mimi naona hivyo ndiyo maana nakuwa mzito" alisema Johari

Aidha Johari amedai kuwa kitendo cha Kanumba kufariki na kuonekana Lulu alihusika kwenye kifo hicho ni jambo ambalo liliwaumiza sana kwa kuwa watu hao wote walikuwa karibu na wao lakini anaamini kuwa yote hayo ni mipango ya Mungu.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad