Klabu ya Simba Yapewa Agizo na Rais

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Klabu ya Simba Yapewa Agizo na Rais

Wachezaji wa Klabu ya Simba imeagizwa kufanya vizuri katika mechi zake anazoendelea kucheza ili iwe njia moja ya wapo ya kumuenzi mchezaji wao wa zamani Mzee Arthur Mambeta aliyefariki jana (Marchi mosi, 2018) Jijini Dar es Salaam.


Agizo hilo limetolewa na maarufu kama 'Try again' wakati alipokuwa anazungumzia jinsi walivyoguswa na taarifa za msiba wa nyota wao zamani kama viongozi wa klabu hiyo.

"Marehemu Mambeta ni hazina ambayo Mungu ametupatia lakini sasa Mwenyezi Mungu mwenyewe amepitisha rehema yake kwa hivyo sisi kama Klabu ya Simba kwa masikitiko makubwa tunawaomba wanachama wetu na wapenzi wa wekundu msimbazi tumuenzi mzee huyu", amesema Salim.

Pamoja na hayo, Salim ameendelea kwa kusema "wachezaji wetu wafanye vizuri  katika mechi zinazokuja ili kumuenzi shujaa wetu huyu kwani ni moja ya wazee wachache waliokuwa wamebaki katika tasnii hii kwa wazee ambao walifanya vizuri na kuitendea mema klabu".

Nyota huyo wa zamani wa Simba, Mzee Arthur Mambeta anatarajiwa kuzikwa siku ya Jumamosi (Machi 3, 2018) katika makaburi ya maeneo ya Buguruni Jijini Dar es Salaam.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad