Sakata la Daimond, Waziri Shonza Lawaibua Wasanii Waomba Kukutana na Mwakyembe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Sakata la Daimond, Waziri Shonza Lawaibua Wasanii Waomba Kukutana na Mwakyembe

Wakati sakata la mwanamuziki Diamond Platinumz kumlalamikia Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza kutowatendea haki wasanii likiendelea kuwa mjadala mitandaoni, Chama wa Wasanii wa Bongofleva (Tuma) kitakutana na waziri wa wizara hiyo, Dk Harrison Mwakyembe wiki hii.

Akizungumza na MCL Digital leo Jumatatu Machi 26, 2018, katibu wa chama hicho, Samuel Andrew maarufu Braton amesema sakata la Diamond na naibu waziri huyo ndio sababu kuu ya kuomba kuonana na Dk Mwakyembe.

Machi 19, 2018 Diamond wakati akihojiwa na Kituo cha Redio Times cha jijini Dar es Salaam, alilaumu hatua ya Serikali kuzifungia nyimbo 15 mwezi uliopita, zikiwamo mbili za kwake.

Diamond hakuishia katika mahojiano hayo yaliyoongozwa na mtangazaji Omary Tambwe, Machi 20, 2018 kupitia mtandao wa Twitter alimjibu naibu waziri huyo akisema ametumia njia hizo kumjibu kwa kuwa naye alitumia hizo hizo.

Katika maelezo yake Braton amebainisha kwamba awali walipanga kuonana na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), kikao ambacho ilikuwa kifanyike leo.

Hata hivyo, amesema baada ya kushauriana na wenzake waliona ni vema kikao hicho akawepo na Dk Mwakyembe kwa maelezo kuwa hata Basata watapeleka taarifa za mazungumzo yao wizarani.

“Unapoongelea waziri ndio mtu wa mwisho kuongea na kutolea uamuzi wa tutakachozungumza, hivyo tukienda Basata ni kama tunazunguka tu wakati kitu tunachohitaji sasa ni utekelezaji na si taarifa,”amesema.

Alipoulizwa kama Shonza atakuwepo kwenye mkutano huo, Braton amesema hana uhakika japo vikao vingi vya wasanii huwa anakuwepo na hata hicho wangependa awepo pia.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad