AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mbunge huyo ameshauri itafutwe suluhu ili kurejesha mahusiano mazuri baina ya makundi hayo.
Akizungumza leo Machi 10, 2018 katika kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa wa Arusha, Lema amesema kama hakuna mahusiano mazuri kwa viongozi si rahisi kuwapatia wananchi maendeleo.
"Hili ni suala la utawala bora, leo hii kuna watendaji wa Serikali wanaogopa hata kupiga picha na wabunge, hasa wa upinzani. Jambo hili linapaswa kuondolewa kwani lina athari katika jamii,” amesema Lema.
Amesema wabunge wana nafasi ya kuchochea maendeleo ya wananchi na kuondoa kero zao, kwamba kuna wakati kiongozi wa serikali kutokana na sababu za kiitifaki hawezi kupeleka hoja moja kwa moja kwa viongozi wa juu lakini mbunge anaweza.
"Tufanye kazi pamoja, leo hii tunapitisha bajeti ya mkoa lakini kama hatuna mahusiano mazuri baina yetu, sisi kama viongozi sidhani kama tutafanikiwa,” amesema.
Akijibu hoja hiyo ya Lema Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Idd Kimanta amesema anaamini viongozi wa Serikali wanajua wajibu wao wa kufanya kazi na wadau mbalimbali.
"Utawala bora ni pamoja na kufanyakazi pamoja na nina imani hili linafanyika lakini kama kuna watu wanatengwa hilo ni jambo la watu binafsi,” amesema.
Hata hivyo, Kimanta ametaka viongozi kufanya kazi ya kutatua kero za wananchi na kuachana na mambo ya siasa kwani chaguzi tayari zimepita sasa ni wakati wa kufanyakazi.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Lema hapa anachokizungumza ni kitu gani? Miswaada ikipelekwa bungeni na Serikali kwa ajili ya Maendeleo wao kila siku kazi yao ni kupinga au wakati mwengine huamua kutoka nje kabisa ya bunge hawataki hata kusikia.
ReplyDelete