AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Bunge la Zambia limemsimamisha waziri kwa muda wa mwezi mmoja asihudhurie vikao kutokana na kosa la kumpiga mbunge kwenye viwanja vya Bunge.
Spika wa Bunge la Taifa, Patrick Matibini amesema Waziri wa Jimbo la Lusaka, Bowman Lusambo amesimamishwa baada ya kumchapa kibao mbunge Chishimba Kambwili hapo Oktoba mwaka jana, na kusema kwamba tabia hiyo haikubaliki dhidi ya mbunge.
"Hili ni Bunge la heshima, nina wajibu wa kuhakikisha kwamba heshima na haiba ya Bunge inalindwa na inahifadhiwa wakati wote," amesema spika huyo.
Kutokana na kusimamishwa huko Waziri Lusambo hatapata marupurupu na mshahara kama mbunge kwa mwezi wote anaotumikia adhabu.
Imeelezwa kwamba ni jambo la kawaida kwa wabunge kutumia lugha isiyofaa na kuleta mizozo, lakini kwa kitendo cha Waziri kumpiga mbunge hakikuwa cha kuvumilika.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK