AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
BARABARA ya Moshi-Dar imefungwa kwa muda asubuhi ya leo eneo la mbele ya Chekereni karibu na daraja la Kileo karibu na Kifaru kutokana na kuanguka mti mkubwa katika barabara hiyo na hivyo kusababisha magari yashindwe kupita.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Hamis Issah, amesema mti mkubwa ulioanguka katika barabara hiyo ulisababisha magari yashindwe kupita na kusababisha foleni pande zote. Vilevile, aliongeza kwamba, katika kugombania kupenya sehemu hiyo, magari mawili makubwa yaligongana katika kutaka kuukwepa mti huo na hivyo kuziba kabisa sehemu yote eneo hilo.
Hata hivyo, alisema, wakati hali hiyo ikiendelea, polisi walifika eneo hilo na kusaidiana na wananchi kuuondoa mti huo kwa kuukata na mapanga na baada ya kukamilika kwa kazi hiyo, magari yaliendelea na safari zao kama kawaida.
Akizungumza na mtandao huu, Kamanda Issah, alisema si kweli kwamba barabara hiyo ilikuwa imefungwa tangu saa 6 za usiku mpaka muda huu, akisema hayo ni maneno ya uvumi na kwamba alichokisema na mtandao huu ndiyo hali halisi.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK