AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Askofu Shoo ametoa kauli hiyo April 1,2018 katika Usharika wa Moshi Mjini Dayosisi ya kaskazini, mkoani Kilimanjaro na kusema kuwa wao wataendelea kusema ukweli siku zote
"Sisi tunasikitika sana tunaposema jambo la kweli, jambo linalohusu maisha ya watanzania wote katika waraka ule tuliotoa kama waraka wa maaskofu halafu kuna watu wachache wajinga mimi nimesema wamesema maaskofu wamesema sababu sadaka zimepungua kanisani, sisi sadaka haijapungua kwani wakristo wameendelea kujitoa sana na hatujapungukiwa na kitu napenda kuwashukuru na Mungu awabariki sana, na sisi tutaendelea kusema ukweli na wanaotaka kuharibu ukweli huo waendelee kuharibu lakini watanzania walio wengi, watanzania wenye hekima wanaelewa maneno tuliyozungumza siyo maneno ya kujibu tu haraka haraka bali maneno ya kututafakarisha"
Askofu Shoo aliendelea kutoa ufafanuzi kuhusu jambo hilo na kusema kuwa
"Tutaitwa majina mengi lakini tunajua ni jitihada za ule upotoshaji wa ule ukweli uliopo katika ule waraka, siyo jambo la hivi hivi tu kwa wakati mmoja maaskofu wa makanisa mawili makubwa hapa nchini kukaa na kutoa waraka, hatukukaa na kusema tutatoa waraka lakini Baraza la Maaskofu wa Katoliki wakakaa na kuja na ule waraka sisi wa KKKT tutakaa tukaja na waraka ukilinganisha ujumbe ni ule ule mimi nasema tena kuna kitu Mungu anataka kutuambia kama Watanzania kupitia ujumbe ule. Mungu awaguse hao wanaotumia nguvu nyingi kutaka kupotosha waraka ule, wanatumia nguvu nyingi kupaka matope"
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK