AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Pia mbunge huyo aliwataka baadhi ya wabunge waache kupiga kelele bungeni juu ya matukio ya watu kupotea na kutekwa, badala yake waviache vyombo vya sheria na vya usalama vifanye kazi yake.
Hayo ameyasema Bungeni wakati akichangia hoja katika Wizara ya Katiba na Sheria jana, Aprili 18, 2018.
“Tuna shida sana na majengo ya mahakama huku kwenye vijiji vyetu Geita ambako tunategemea watu wanakwenda kutendewa haki huko, lakini mahakama ni chache na zilizopo unakuta kuna popo, lakini pia zimejaa mahabusu. Ningeomba waziri alete mapendekezo tubadilishe sheria ili ambao wana makosa madogo wapigwe hata makofi tu na waachiwe,” alisema Msukuma.
Akizungumzia mauaji na utekaji, Msukuma alisema:
“Sisi kama wabunge tunaotunga hizi sheria tuviache vyombo vifanye kazi yake, hawa wanaosema sijui nani kapotea mara Beny Saanane, hata watu wa CCM wamepotea wengi tu, wamechinjwa Kibiti wengi tu, na hatukupiga kelele, tumeviachia vyombo vinalishughulikia.
“Mimi nilikuwa kwenye kampeni za uchaguzi mdogo pale Kinondoni, nani hajui kama mlikuwa mnasema kwamba watu waandamane na mbebe majeneza mia mbili? Ungekuwa wewe serikali ungeacha watu waandamanae wafe? Tuviachie vyombo vifanye kazi yake, hata mimi nilifanya kosa na niliwekwa ndani. Hawa wakorofi wakifanya makosa wawekwe magerezani, unamuona Lema sasa hivi kidogo amekuwa binadamu.”
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK