Serengeti Boys watinga Nusu Fainali CECAFA U17

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


TIMU ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys imepata ushindi mnono wa mabao 6-0 dhidi ya Sudan katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA U17 inayoendelea nchini Burundi.

Kwa matokeo hayo, Serengeti Boys inakwenda Nusu Fainali ya michuano hiyo kutoka Kundi B, ikiungana na Uganda, zote zikiwa na pointi nne kila moja, wakati Sudan inaaga baada ya kupoteza mechi zote mbili.

Zanzibar ni timu nyingine iliyopangwa katika kundi hilo, lakini iliondolewa kwa kuwasili na wachezaji waliozidi umri.

Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Muyinga mjini Bujumbura, mabao ya Serengeti Boys yamefungwa na Alphonce Msanga mawili dakika za nne na 59, Mustapha Nankunku dakika ya 27, Edson Mshirakandi dakika ya 28, Jaffar Mtoo dakika ya 78 na Kelvin Paul dakika ya 83.

Mechi yake ya kwanza, Aprili 15, mwaka huu Serengeti Boys ilitoa sare ya 1-1 na Uganda.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad