AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mtandao wa Twitter ingawa inavutia mazungumzo mbalimbali kuanzia ya kisiasa, kiutani, n.k yanayohusisha hadi watu mashuhuri kama Rais wa Marekani wa sasa, wasanii na watu wengine mashuhuri kwa wadogo bado mtandao huu unapata shida katika kuvutia makampuni kutumia pesa kujitangaza katika mtandao huo.
Mtandao wa Twitter bado upo nyuma katika kuvutia mapato yanayotokana na matangazo ukilinganisha na mitandao mingine kama vile Facebook na ata Instagram na Snapchat.
Katika ripoti ya mapato na ukuaji ya kampuni uya Twitter iliyotoka Alhamisi hii inaonesha bado mtandao wa kijamii wa Twitter unapata shida kukuza idadi ya watumiaji, matangazo na mapato.
Kwa mfano katika miezi mitatu ya mwisho ya mwaka 2016 Twitter ilikuwa na wastani ya watumiaji milioni 319 kwa mwezi, huu ni ukuaji wa asilimia 4 tuu ya watumiaji ukilinganisha na kipindi cha mwaka mmoja nyuma, pia namba hii ni ndogo ukilinganisha na mtandao wa Facebook. Facebook ina takribani wastani wa watumiaji bilioni 1.86 kwa mwezi.
Twitter wanategemea kupata mapato ya dola milioni 91 tuu katika kipindi cha miezi hii mitatu ya mwanzo, hii ni chini sana ukilinganisha na pato la dola milioni 191 ambalo wengi waletegemea wafikie.
Ingawa bado kibiashara mtandao huo upo katika hali ngumu ila ni uhakika bado hautaenda popote kwa sasa. Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Bwana Jack Dorsey anasema itaitaji muda mrefu kidogo na mabadiliko kadhaa ili kuweza kuona ukuaji wa watumiaji pamoja na mapato
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK