Zitto Kabwe: Sisi wanakigoma tunasema Kigoma kwanza kabla ya Tanzania

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Dodoma. Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT -Wazalendo), Zitto Kabwe amemtaka waziri wa Tamisemi kulitafutia ufumbuzi suala la kutoweka kwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kakonko, Simon Kangue.

Amesema hayo bungeni leo Aprili 12, 2018 alipochangia mjadala wa hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Rais, yenye wizara za Tamisemi; na Utumishi na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2018/19.

“Habari zinazosambaa Kibondo tayari ameuawa. Tunataka maelezo ya mtu huyo, sisi watu wa Kigoma ni Kigoma kwanza kabla ya kuwa Watanzania naomba hilo mlielewe,” amesema.

Zitto amesema mara ya mwisho kuonekana mwenyekiti huyo aliitwa kwa mkurugenzi na kukutana na ofisa usalama wa wilaya.

Amesema tangu siku hiyo hajulikani alipo mwenyekiti huyo licha ya jitihada za kumtafuta kufanyika.

“Familia imechukua hatua mbalimbali, imelalamika na sisi wajumbe wenzake tumehoji kwenye vikao, hakuna maelezo yoyote kutoka serikalini,” alisema Zitto.

VIDEO:


Chanzo: Mwananchi
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad