Mahakama Yaibana Serikali kesi ya mhasibu Takukuru

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imetoa siku 14 kwa upande wa mashtaka kuhakikisha wanakamilisha kuchapa maelezo ya washtakiwa wa kesi ya kumiliki mali zisizoendana na kipato, inayomkabili mhasibu mkuu wa Taasisi na Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Godfrey Gugai na wenzake watatu.

Mbali na Gugai, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni George Makaranga, Leonard Aloys na Yasini Katera na wote wanakabiliwa na mashitaka 43 yakiwemo 20 ya utakatishaji wa fedha haramu, kumiliki mali zisizoendana na kipato na kughushi mikataba ya mauziano ya viwanja katika maeneo mbalimbali.

Uamuzi huo umetolewa leo Mei 16, 2018 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba baada ya kesi hiyo kuahirishwa kwa zaidi ya mara saba,ikiwa katika hatua ya kuwasomea hoja za awali (PH), washtakiwa hao.

Hatua hiyo, inatokana na upande wa mashtaka kuieleza Mahakama hiyo kuwa wapo katika hatua za mwisho za kuchapa maelezo ya washtakiwa.

Awali, wakili wa Serikali Mkuu, Vitalis Peter amedai mahakamani hapo kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya washtakiwa kusomewa maelezo ya awali, lakini walikuwa hawajakamilisha uchapaji wa maelezo ya washtakiwa hao.

“Kesi imekuja kwa ajili ya upande wa Jamhuri kuwasomea maelezo ya awali washtakiwa wote , lakini tunaiomba Mahakama itupe ahirisho la mwisho ili tuweze kukamilisha uchapaji wa maelezo ya washtakiwa,” amedai wakili Peter.

“Tayari maelezo ya washtakiwa tumeshaanda na kilichobaki ni kuchapwa tu, hivyo tunaiomba Mahakama yako itupe ahirisho la mwisho.”

Baada ya maelezo hayo, wakili wa utetezi, Semi Malimi na Alex Mgongolwa wamedai kuwa maelezo ya awali yameahirishwa kusomwa kwa zaidi ya mara saba kuanzia April 4, 2018.

Baada ya kupitia maelezo ya pande zote, hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Mei 30, 2018 na kuutaka upande wa mashtaka kuhakikisha wanakamilisha kuchapa maelezo hayo ili washtakiwa hao waweze kusomewa maelezo ya awali.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad