Siku Nikki wa Pili Akipewa Uwaziri Atafanya Jambo Hili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Siku Nikki wa Pili Akipewa Uwaziri Atafanya Jambo Hili
Msanii wa muziki wa hip hop Bongo, Nikki wa Pili amesema ili wasanii watambulike kama wafanyakazi ni lazima serikali itambue wasanii wanafaje kazi na iwapo wanataka kuilinda ijue inalinda kitu gani.

Amesema baada hapo kinaweza kuanzishwa chama cha wasanii wafanyakazi ambacho kinasimama na kutengeneza kanuni na taratibu za mfanyakazi huyo na kitu hicho kutafsiriwa kama sheria.

“Kubadilisha sanaa kuwa biashara hicho ni kitu kingine, so niwajibu wa msanii kujifunza misingi ya biashara, hiki nilichonacho mkononi ninawezaje kukiuza? . Ukinipa uwaziri kitu cha kwanza ni kufanya utafiti mkubwa wa biashara ya muziki,” amesema.

“Kujua hii biashara inafanyikaje, uhalisia wake ni upi na huo uhalisia wake umetengeneza picha gani, then kutoka hapo tunawezaje kwenda mbele, bila kutafiti kwa facts utapiga bla! bla!,” Nikki wa Pili amesema hayo katika mahojiano na JJ wa Jembe FM.

Nikki wa Pili kutoka kundi la Weusi kwa sasa anatamba na ngoma Hesabu ambayo amemshirikisha producer, S2kizzy.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Top Post Ad