Vitendo vya Uharamia Viliongezeka Mwaka 2017

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Vitendo vya Uharamia Viliongezeka Mwaka 2017
Idadi ya vitendo vya uharamia pwani ya Afrika mashariki iliongezeka mara mbili mwaka 2017 ukilinganisha na mwaka 2016, Vyombo vya kimataifa vinavyoshughulikia usalama wa majini vimeeleza.

Ilioyesha kuwa mtandao wa uhalifu nchini Somalia ulikuwa bado una uwezo wa utekeleza mashambulizi.

Vitendo vya uharamia mwaka 2017 vinaonyesha wazi kuwa makundi haya yameendelea kuwa na uwezo wa kuratibu na kutekeleza mashambulizi dhidi ya Meli zinazosafiri kwenye eneo la Afrika .

Phil Belcher kutoka kwenye taasisi ya Intertanko amesema mgogoro nchini Yemen pia ulikuwa ukitishia usafirishaji wa majini karibu na eneo la pembe ya Afrika

''Tunawashauri washirika wetu kuja na mbinu madhubuti za kiusalama ili kudhibiti vitisho vingine.

Maharamia waiteka meli huko Somalia

Uharamia umeendelea kuwa tishio katika rasi ya Guinea ingawa hatua mbalimbali zimechukuliwa katika maeneo ya pwani na makampuni ya ulinzi wa majini, imeeleza ripoti hiyo

Meli ya Korea Kusini Munmu ili tumwa tena katika eneo la rasi ya Guinea baada ya wavuvi watatu wa Korea Kusini kutekwa mwezi Machi.Utekaji nyara kwa ajili ya kujipatia pesa umeendeleza kukumba eneo hili, ambapo imezoeleka kuwa hivyo kwa bahari mbaya kuanzia mwaka 2016, alieleza Maisie Pigeon,mwandishi wa ripoti hiyo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad