Waziri wa Nishati Amuomba Mungu Ailaze Serikali Mahali Pema Peponi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani amewavunja mbavu wabunge baada ya kuwaambia anamuomba Mwenyezi Mungu aiweke serikali mahala pema peponi.

Dk. Kalemani ametoa kauli hiyo bungeni jijini Dodoma leo Mei 25, alipokuwa akihitimisha mjadala wa Bajeti ya Wizara yake kwa mwaka wa fedha 2018/19 aliyowasilisha jana.

Kabla ya kusema hayo Dk. Kalemani alikuwa akieleza jinsi serikali ilivyotekeleza miradi mbalimbali na kuwapelekea wananchi umeme katika maeneo mbalimbali nchini ambapo alijikuta akisema: “namuomba Mwenyezi Mungu aiweke serikali mahali pema peponi,”.

Hatua hiyo iliwafanya wabunge kuangua vicheko huku Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu akilazimika kuwatuliza wabunge na kuwataka waendelee kumsikiliza waziri badala ya kucheka.

Hata hivyo, baada ya dakika chache Dk. Kalemani alisema anamuomba Mwenyezi Mungu aibariki serikali na kuwafanya wabunge kucheka tena kwa sauti.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad