Ajali yaua Watano na Kujeruhi Watu Watatu Mkoani Mtwara

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Ajali yaua Watano na Kujeruhi Watu Watatu Mkoani Mtwara
Ajali mbaya imetokea mkoani Mtwara na kusababisha vifo vya watu watano na watatu kujeruiwa baada ya gari aina ya Toyota Noah walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kupinduka, kisha kuwaka moto.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Lucas Mkondya amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa ajali hiyo ilitokea jana saa 10 jioni katika kijiji cha Chingweje wilaya ya Nanyumbu mkoani hapa.

 Kati ya waliofariki dunia ambao wametambulika ni dereva wa gari hilo Babuu Maroro
huku maiti nyingine wameshindwa kutambulika baada miili yao kuungua na moto.

Amesema  majeruhi wa ajali hiyo waliolazwa katika Hospitali ya Mkomaindo Masasi ni Daria Bushiri (30) mkazi wa Masuguru, Afkam Ling'ande (4) na Khalid Salum  ambaye ni kondakta wa gari hilo.

“Lilivyoanza kuwaka moto, watu watatu walitoka salama ila watano walioshindwa kutoka waliungua, kati yao wawili wameungua vibaya na hawatambuliki. Watatu kidogo wanaweza kutambulika. Tunaomba ndugu jamaa kujitokeza kutambua miili ya marehemu ambayo imehifadhiwa katika hospitali ya Mkomaindo.”



----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Top Post Ad