AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi Kadi hizo Makonda amesema kuwa kadi hizo zimefadhiliwa na Hospital ya Regency na TMJ za jijini Dar es Salaam na zitakuwa na ndani ya mwaka mmoja kuanzia sasa walipokabidhiwa.
Aidha pamoja na hayo Makonda amesema watoto wengine 400, watapatiwa msaada wa mabegi yenye vifaa vyote vya shule.
"Kupitia mwezi huu wa ramadhani nawashukuru ndugu zetu wa Regency na TMJ kwa kwa msaada mkubwa wanaoutoa angalau kugusa maisha ya watoto yatima, hivyo leo tumekutana ili kuonesha ishara ya amani upendo pamoja na undugu bila kujali itikadi za vyama na dini" amesema Makonda
Kwaupande wake Kaimu Mganga mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Daisy Majamba amesema Jumla ya Card 220 zimekabidhiwa, na kwamba kupatikana kwa watoto hao kulifanyika zoezi la kuwa tambua kutoka katika vituo mbalimbali vya kuelekea watoto jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Hospitali ya Regency Medical Center Dr Rajni Canabar amemshukuru mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe Makonda kwa kuanzisha mchakato wa kumgawa Card hizo na wao kama wadau wamefurahi kushiriki katika kusaidia watoto hao na kuitaka jamii kuwa thamani na kuwa linda watoto hao na kuwa ona sawa na wengine.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi gharama matibabu ya Toto Afya Kadi ambazo ni kila moja ni shilingi 50400, kwa mwaka ni nafuu ukilinganisha na gharama za matibabu bila kadi hiyo.
Aidha ameitaka kutambua umuhimu wa Afya kwa Watoto wao kwa kuwa Katia Toto Afya Kard, na kuwataka wadau wengine kujitokeza kuzihuisha kadi hizo baada ya muda wake kwisha.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK