AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Usajili wa sasa utakuwa tofauti na ullivyozoeleka miaka ya nyuma ambapo msimu ujao watatumia mfumo mpya ujulikanao kwa jina la TFF FIFA CONNECT.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa TFF, Clifford Ndimbo, alisema mfumo huu utafafanuliwa zaidi katika semina ambazo zitaendeshwa kwa kuwahusisha viongozi wa klabu zote za Ligi Kuu, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili.
Ndimbo alisema kuwa semina hizo zitaanza mapema kabla ya kuanza kutumika ili kutoa uelewa sahihi wa namna unavyopaswa kutumika kwa timu zote husika.
"Semina ya kwanza itaanza kwa timu zinazoshiriki Ligi Kuu Bara ambayo itafanyika Jumatatu ya Juni 25 mwaka huu, halafu itaendelea tena kesho yake itakayokuwa Jumanne kwa zile timu za Ligi Daraja la Kwanza na Jumatano utahusisha klabu za ligi Daraja la Pili," alisema Ndimbo.
Aliongeza kuwa, kutokana na mabadiliko ya mfumo huo wa usajili, TFF imeweka muda wa wiki moja kwa ajili ya kuweka mapingamizi endapo yatakuwepo ambapo klabu zinatawasilisha kupitia kamati maalum itakayosimamia suala la usajili huo.
"Tunawaomba viongozi wa klabu zote kuzingatia muda wa mafunzo ya juu ya mfumo huo mpya ili kuepusha matatizo ambayo yanaweza yakajitokeza baadaye," alisisitiza Ndimbo.
Aliweka wazi kuwa dirisha la usajili tayari lilishafunguliwa tangu Juni 15 na litafungwa ifikapo Julai 26 mwaka huu.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK