Viongozi wa Ethiopia na Eritrea Wamekubaliana Kukutana

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Viongozi wa Ethiopia na Eritrea Wamekubaliana Kukutana
Viongozi wa Ethiopia na Eritrea wamekubaliana kukutana kwa mara ya kwanza katika muda wa takribani miaka 20 ishara ambayo haikutegemewa ya kuanza upya uhusiano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili jirani kwenye pembe ya Afrika.

Waziri wa mambo ya nje wa Ethiopia, Workneh Gebeyehu aliliambia shirika la habari la Associated Press-AP siku ya Alhamis kwamba mkutano huo utajenga msingi bora wa kurejesha amani. Aliongeza kuwa muda na mahala ambako mkutano utafanyika bado haujajulikana.

Mwanadiplomasia wa juu wa Ethiopia alizungumza wakati ujumbe wa Eritrea ulio-ongozwa na waziri wa mambo ya nje, Osman Saleh kumaliza ziara ya siku tatu ya kihistoria huko Ethiopia.

Mahusiano mabaya ya nchi hizo mbili yalianza wakati vita vya mpaka vilipotokea mwaka 1998 miaka mitano baada ya Eritrea ilipojinyakulia uhuru wake kutoka Ethiopia.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Top Post Ad