AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mapema tu baada ya Mkutano Mkuu wa Klabu ulifanyika Juni 10 kwenye Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oyster Bay, walikusanyika na daladala mbili kwenda moja kwa moja katika makazi ya Manji.
Mara baada ya kuwasili taarifa zinaeleza hawakufanikiwa kumkuta na badala yake walikutana na mlinzi aliyewaambia kuwa bosi wake hayupo akieleza amesafiri. Wanachama hao ilibidi wamwachie ujumbe mlinzi huyo wakiomuomba amwambie kuwa bado anahitajika katika kiti cha Uenyekiti ndani ya klabu.
Hatua hiyo imekuja mara baada ya Manji aliyetarajiwa kufika kwenye mkutano huo kushindwa kuwasili na kuleta sintofahamu kama anaweza akarejea kwenye nafasi yake.
Ikumbukwe Maji alijiuzulu nafasi ya Uenyekiti Mkuu Yanga kwa maelezo ya kuwa alikuwa anahitaji kupumzika na badala yake nafasi yake ikawa chini ya Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi ya TFF.
Katika Mkutano Mkuu uliofanyika Juni 10 jumla ya wanachama 1,400 waliohudhuria walipinga barua ya Manji iliyosema amejiuzulu na kuazimia moja kwa moja kuwa ataendelea kusalia kama Mwenyekiti wao.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK