AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
kufanya hivyo kwa kuwa wanaingiza kipato kikubwa kutumia tangazo hilo.
Hayo yamebainishwa leo Julai 10, 2018 na Katibu Mtendaji wa BASATA, Godfrey Mngereza pamoja na Mkuu wa Matukio, Kwerugira Maregesi wakati wakizungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo 'PB' inayorushwa kupitia East Africa Radio baada ya kuwepo malalamiko mengi ya wasanii wakidai kanuni hizo mpya haziwatendei haki kwa kile walichokuwa wakiamini kwamba wanapaswa kuilipa BASATA milioni tano kwa kila kazi ya tangazo watakayokuwa wanaifanya na kampuni yoyote ile nchini bila ya kuangalia kiasi wanachokiingiza wao binafsi.
"Hayo makampuni yakifanya matangazo kupitia msanii wanatengeneza fedha nasio kitu cha bure bure tu. Pia hayo makampuni yalikuwa yanafanya kazi na wasanii hao kinyume na sheria bila ya kufahamika na BASATA. Kwa hiyo sasa hivi tutawatambua", amesema Mwingereza.
Pamoja na hayo, Mwingereza ameendelea kwa kusema "milioni tano inalipwa na kampuni husika na wala sio msanii ambaye ametumika kufanya tangazo fulani kwa kampuni".
Mbali na hilo, Mwingereza amesema kuwa sio kweli kwamba walifanya mabadiliko hayo mapya bila ya kuwashirikisha wadau wa muziki kwa kuwa jambo lolote la serikali haliwezi kufanikiwa bila ya kuwepo na maoni.
"Hizi kanuni zisingeweza kutoka kama zisingekuwa na ushirikishwaji, hakuna 'document' ya serikali inayotoka bila ya kuwepo na ushirikishwaji wa wadau. Kuna changamoto ya watu ya kutosema ukweli nchi hii", amesisitiza Mwingereza.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK