AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Taarifa za Chelsea kutaka saini ya Cech zimekuja muda mfupi baada ya Arsenal kufungua milango kwa kipa huyo.
Kocha mpya wa Chelsea, Maurizio Sarri, amegoma kumpigia magoti kipa Thibaut Courtois anayetaka kujiunga na Real Madrid katika usajili wa majira ya kiangazi.
Sarri ameweka mezani majina ya makipa watatu akiwemo Cech, aliyecheza mechi 333 Chelsea kurejea katika klabu hiyo.
Makipa wengine wanaotupiwa jicho na Sarri ni kipa wa Leicester City Kasper Schmeichel na chipukizi wa AC Milan, Gianluigi Donnarumma mwenye miaka 19.
Sarri anaamini Cech atakuwa radhi kurejea Chelsea baada ya kocha mpya wa Arsenal, Unai Emery kumponda siku chache baada ya kutia saini mkataba wa kuifundisha timu hiyo na tayari amemsajili kipa wa Bayer Leverkusen ya Ujerumani, Bernd Leno mwenye miaka 26.
Sarri ametua Chelsea kujaza nafasi ya Mtaliano Antonio Conte aliyetupiwa virago baada ya kushindwa kuipa mafanikio katika mashindano ya Ligi Kuu England msimu uliopita. Licha ya kuipa ubingwa Chelsea katika msimu weke wa kwanza, Conte aliibua mzozo baada ya kumtimua Diego Costa.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK