AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kocha huyo, alitua nchini wiki mbili zilizopita na kuanza kibarua cha kukinoa kikosi hicho kwa ajili ya Kombe la Shirikisho Afrika akichukua nafasi ya aliyekuwa kocha msaidizi wa timu hiyo, Shadrack Nsajigwa aliyemaliza mkataba wa kuifundisha timu hiyo mwishoni mwa msimu uliopita wa Ligi Kuu Bara.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Jumatano, kocha huyo aliondoka nchini baada ya kushindwa kufikia muafaka masuala ya kimkataba na viongozi wa Yanga kabla ya kubeba mabegi yake na kurudi kwao.
Mtoa taarifa huyo alisema, kocha huyo ana wiki mbili tangu ameondoka kwenye timu hiyo iliyokuwa inajifua kwenye Uwanja wa Chuo cha Polisi, Kurasini jijini Dar es Salaam.
“Nashangaa kuona hadi sasa mmekuwa kimya, kocha Mcongo aliyekuja kuwa msaidizi wa Zahera sasa ni wiki mbili hayupo hapa nchini.
“Hivyo, kocha Zahera hivi sasa yupo peke yake anakinoa kikosi hicho akishirikiana na kocha wa viungo Mwandila (Noel), baada ya kuondoka huyo mpya.
“Kikubwa kocha huyo alishindwa kufikia muafaka mzuri na mabosi wake hao ya kusaini mkataba wa kuifundisha Yanga,” alisema mtoa taarifa huyo.
Alipotafutwa Zahera kuzungumza kuzungumzia hilo alisema kuwa :“Sifahamu taarifa za kuondoka Yanga kwa kocha huyo, nilikuwa naye kwa kipindi fulani, lakini siku za hivi karibuni sijamuona uwanjani.”
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK