AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23 aliyesajiliwa kutoka katika klabu ya RB Leipzig ya nchini Ujerumani kwa uhamisho wa ada ya Euro mil 57,tayari amekabidhiwa jezi yeye namba 8 mgongoni ambayo alikuwa akiivaa mkongwe huyo ambaye kwa sasa ni kocha katika klabu ya Rangers.
akiongea na kituo cha Espn Keita amesema “Baba yangu alizungumza na mimi nilipojiunga na Liverpool na amenieleza jinsi gani anavyoipenda Liverpool hata sisi wakati tunacheza mpira mtaani tulikuwa tukivaa Jezi za Liverpool.”
Keita ameongeza “Kwa sababu mimi ni kiungo na Gerrard pia alikuwa kiongozi katika upande huu, haiwezi kuwa mtu mwingine yeyote isipokuwa Steven Gerrard ambaye ningependa kwa wakati huu wote ninapokuwa nacheza, nataka kuwa kama yeye”
keita amemaliza kuwa kamwe hataiangusha hadhi ya Jezi namba 8 na anataka kuvaa viatu vya Gerrard ipasavyo.na alishtushwa sana na maneno ya Gerrard aliposema kuwa “Kila mtu yuko hapa kukusaidia ili uweze kuiendeleza namba 8.”huku akimaliza kuwa “Ninajua ni namba kubwa hapa na ninafurahi sana kuivaa lakini pia ni kitu ambacho sitakiwekea shinikizo lolote zaidi.”
Liverpool wamefanikiwa kufanya usajili mzuri katika maeneo tofauti tofauti kwa lengo la kukisuka kikosi baadhi ya sajili ambazo wamezifanya ni pamoja na kuwasajili ( Naby Keita – kutoka Leipzig, £52.75m, Fabinho – kutoka Monaco, £43.7m, Xherdan Shaqiri -kutoka Stoke, £13.5m, Alisson Becker – kutoka Roma, £67m na Isaac Christie-Davies – kutoka Chelsea, bure.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK