AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizunguma na wanahabari jana Agosti 2, Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma Gilles Muroto, alisema ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia jana wilayani Bahi, Dodoma kwenye barabara kuu ya Singida-Dodoma.
Waliofariki ni watoto Yusra Salum (5), Karialino Hamis (2), Hussein Hamisi (miezi miwili) na Mfaume Hamis (30) ambaye alikuwa dereva wa bodaboda.
Kamanda Muroto amesema mwendesha pikipiki huyo alikuwa amewapakia watoto watatu na mama yao na aliingia barabarani ghafla na pikipiki hiyo iligongwa na basi la kampuni ya Satco.
Muroto ameeleza kuwa basi hilo lilikuwa likitokea Mwanza kuelekea jijini Dar es salaam.
“Kwenye hiyo pikipiki walikuwa wamepanda jumla ya watu watano, watoto watatu na mama yao dereva amefariki dunia papo hapo na watoto watatu mama huyo na mama mwenyewe naye ni majeruhi hospitali,”alisema.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK