Jeshi la Polisi Lasema Mbwa Aliyedaiwa Kupotea Alikuwa Kwenye Mafunzo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mbwa wa kazi maalum za Bandari ya Dar es Salaam anayedaiwa kutoweka katika mazingira ya kutatanisha, alikuwa kwenye mafunzo bwalo la Polisi.

 Hayo yameelezwa leo Agosti Mosi na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa katika mkutano na wanahabari. Amezungumza hayo huku ukumbini hapo kukiwa na mbwa wawili wa polisi, akiwamo anayedaiwa kutoweka.

Amesema kulikuwa na mkanganyiko na hakuna mbwa aliyepotea.

“Tunataka kuwaambia kuwa mbwa huyo alikuwa kwenye mafunzo ya bwalo la Polisi na mbwa aliyekuwa hayupo siyo hobi,” amesema Mwakalukwa na kuongeza:

“Mbwa wote wapo hakuna hata mmoja aliyetoweka huwa wanaenda kwenye kazi na kurudi.”

 Julai mwaka huu, Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola alimpa saa saba Mkuu wa Jeshi la Polisi, (IGP) Simon Sirro kuhakikisha mbwa huyo anarudi bandarini baada ya kupotea katika mazingira ya kutatanisha.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad