AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Uwoya ameileleza MCL Digital leo Ijumaa Agosti 10, 2018 kuwa Mzee Majuto alipokuwa akipatiwa matibabu hospitalini hapo, alimuita aende kumuona.
Majuto alifariki dunia Agosti 8, 2018 akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali. Anatarajiwa kuzikwa leo kijijini kwake Kiruku mkoani Tanga.
Akizungumzia msiba wa nguli huyo wa vichekesho nchini, Uwoya amesema ameacha pengo kubwa katika tasnia ya uigizaji na Taifa.
Amesema kinachomsikitisha zaidi ni kutokwenda kumjulia hali Majuto, “yaani naumia na wala sijui nielezeje, mbaya zaidi hata pale alipokuwa akiumwa na kulazwa hospitali kwa nyakati tofauti nilishindwa kwenda kumuona pamoja na kwamba alishanipigia simu mara mbili niende lakini sikufanya hivyo.”
“Nilikuwa na majukumu mengi kwa kweli na kuna kipindi nilikuwa na nafasi lakini sijui nini kilichokuwa kinanifanya nishindwe kwenda, hii kitu itaendelea kuniumiza kwakweli.”
Akimzungumzia namna walivyoishi na Majuto, amesema alikuwa ni zaidi ya msanii na walimchukulia kama baba yao, babu yao na yeye alishaenda hadi nyumbani kwake Tanga.
Amesema marehemu atakumbukwa kwa kutopenda kujikweza na kuheshimu mashabiki na watu wengine.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK