Hamissa Mobeto Yamemfika Hapa Aandika Waraka Mzito Kujivua Gamba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Hamissa Mobeto Yamemfika Hapa Aandika Waraka Mzito Kujivua Gamba
Mwanamitindo na mjasiriamali ambaye pia ni mzazi mwenzake na Diamond Platinumz, Hamisa Mobetto, kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika waraka mzito kuhusiana na historia ya maisha yake.

Alichokiandika kupitia ukurasa wake:

“Pengine hufahamu alipotoka Hamisa Mobetto… Wacha nikufahamishe, nilianza kutambulika rasmi kwenye tasnia ya urembo mwaka 2010 baada ya kuibuka mshindi wa Miss XXL After School Bash. Njia ya mafanikio ilifunguka hapo na hatimae nilishiriki Miss Tanzania na Also Miss New World Tanzania Na Kua first Runner Up 2012.


Lakini Pia Nilifanikiwa Kushriki Miss UniAfrica na kuingia Top Ten… Safari ikaendelea na kwa kuwa urembo ni kipande cha sanaa niliingia kwa pia kwenye Bongo Movie na kucheza filamu kadhaa na huku pia nikiwa Video Vixen kwa baadhi ya nyimbo za Bongo Fleva… Nisieleweke vibaya kwa hili, kitanda hakizai haramu… nilipata mtoto wangu wa kwanza miaka michache iliyopita na ninashukuru katika mahusiano yale nilipendwa mimi na mwanangu na kuhudumiwa kwa kila kilichohitajika baadae tena nikapata mtoto mwengine katika mahusiano mengine ambayo pia yalikuwa mazuri na huduma zote kama kawaida zilikuwepo na zinaendelea kuwepo mpaka sasa… Shukrani kwa baba wote wa watoto wangu.



Huyo ni mimi Hamisa Mobetto, safari hiyo imenifundisha mengi sana mpaka sasa na nafikiri nimekomaa kwa kiasi fulani… Nashukuru Hamisa Mobetto imekuwa Brand kubwa mpaka kufikia kunipa ‘Deals’ mbalimbali zinazoendelea kuja (Alhamdullilah). Sio tu ‘Deals’ pekee bali hata fanbase imekuwa kubwa mno kitu ambacho ninakifurahia kwani ni Support kubwa sana ninaipata. Wapo walioamua kutengeneza page za Social Media mbalimbali kwa ajili ya kuonyesha support na wengine pia kutumia fursa hiyo kutengeneza ajira kupitia matangazo n.k nasemaje Yote Heri!


Dunia inaenda mbele na watu wanabadilika, pengine lifestyle ya zamani haikuwa nzuri na mpaka kusababisha ‘mambo flani flani’ kutokea katika maisha yangu lakini umri unapozidi kusonga mbele akili inatanuka na kujifunza mambo mengi kwenye maisha.


Hamisa wa sasa sio kama yule wa zamani, nimezidi kuwa na akili yenye kupambanua mabaya na mazuri na kuchukua hatua ili kuenda na kasi ya ukuaji wa akili yangu. Namshukuru Mungu ananiongoza vyema na naona baraka anazonipatia.

Nimeingia katika migogoro ya hapa na pale kama kutukanana na watu kwenye mitandao na yote hayo ni aidha kwa kufahamu au kutofahamu lakini kwa kuwa yamepita basi niyaache tu na niendelee na safari ya maisha nikiwa mpya kabisa. Fanbase nayo haikuniacha ilikuwa na mimi wakati wote huo kama ugomvi basi walipigana kwa ajili yangu.


Lakini pia inawezekana niliwahi kuwakwaza watu kwa mambo yangu, nichukue fursa hii KUWAOMBA SAMAHANI na kuwaahidi kuwa haitokuja kutokea tena kwa sababu Hamisa wa sasa nimebadilika na ndio maana sitahitaji tena kuingia kwenye ugomvi wa aina yoyote na mtu yeyote yule katika maisha yangu na pia niwaombe mashabiki zangu na Fanbase kwa ujumla iwe kwenye groups za whatsapp au pages za kwenye social media kutojihusisha na ugomvi au matusi na mtu yeyote atakaetaka ugomvi na mimi na badala yake nguvu kubwa iwe kwenye kuendelea kuni’support kwa nguvu kubwa. Nia yangu ni kutowaingiza wale wanaonipenda katika matatizo kwa sababu hawastahili hata kidogo kupata shida kwa sababu yangu. Ninawapenda mno

Namalizia kwa kurudia tena ‘Dunia inaenda mbele na watu wanabadilika’

#NewHamisa
#NewLife

Asante na barikiwa sana!


HABARI ZAIDI KAMA HIZI SOMA KUPITIA APP YA UDAKU SPECIAL

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad