AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kwa mujibu wa mtandao wa habari wa BNN Bloomberg, kampuni hiyo itashirikiana na kampuni mwenyeji ya kutengeneza bangi kwa jina Aurora Cannabis.
Lengo kuu la kuwa na kinywaji hicho litakuwa ni kupunguza maumivu na si kuwalewesha watu.
Kampuni hiyo bado haijazungumzia hadharani mpango huo lakini imekiri kwamba inafuatilia kwa karibu matukio katika sekta ya vinywaji vyenye bangi.
"Kwa pamoja na wadau wengine wengi katika sekta hii ya vinywaji, tunafuatilia kwa karibu ukuaji wa soko la vinywaji vyenye bangi aina ya cannabidiol visivyolewesha kama kiungo katika vinywaji vya kuboresha afya maeneo mengi duniani," taarifa ya Coca-Cola imesema.
Cannabidiol, ni moja ya viungo vinavyopatikana ndani ya bangi, na inaweza kusaidia kupunguza kuvimba, maumivu na kuganda kwa misuli.
Hatua ya Coca-Cola inajiri huku Canada ikijiandaa kuyafuata baadhi ya majimbo ya Marekani ambayo majuzi yameidhinishwa matumizi ya bangi kwa sababu za kujiburudisha, baada ya kukubali matumizi ya bangi kwa sababu za kimatibabu kwa miaka mingi.
Hatua hiyo imechangia kuibuka kwa biashara kubwa ya ukuzaji wa bangi, pamoja na kuundwa kwa ushirikiano wa kampuni kubwa katika biashara hiyo.
Mikebe ya Coca Cola yagunduliwa kuwa na kinyesi cha binadamu
Chupa ya mvinyo ghali zaidi duniani yaibwa Denmark
Mapema mwaka huu, kampuni kubwa ya utengenezaji wa bia ya Molson Coors Brewing ilitangaza kwamba itakuwa ikitengeneza vinywaji vyenye bangi kwa ushirikiano na kampuni ya Hydropothecary, huku kampuni inayotengeneza bia ya Corona, Constellation Brands, ikiwekeza zaidi ya $4bn zaidi katika kampuni ya bangi ya Canopy Growth.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK