AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Savage, 38, amelalamika kwamba pia alikosa gari la kumsafirisha kwenda uwanja wa ndege kama ilivyokuwa matarajio.
Anaonekana kugundua kwamba bili ya malazi haikuwa imelipiwa yote wakati wa kuondoka hotelini.
Savage, ambaye jina lake kamili ni Tiwatope Savage-Balogun, alikuwa amezuru Kenya kutumbuiza katika hafla ya uzinduzi wa almabu mpya ya mwanamuziki nyota kutoka Kenya kwa jina Redsan siku ya Jumamosi. Mwanamuziki wa Jamaica Demarco pia alitumbuiza.
Uzinduzi wa albamu hiyo kwa jina Baddest ulifanyika katika mghahawa maarufu wa Carnivore, na hafla hiyo ilitangazwa sana kwenye mitandao na vyombo vya habari.
Savage amesema alijaribu kumpigia simu promota aliyekuwa amemwalika kuja Kenya bila mafanikio.
Aliwatetea wasanii akisema hawawezi kulaumiwa kwa kulalamika kila mara kuhusu mapromota, iwapo matukio kama hayo yatafanyika.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK