Waziri Mkuu Asitisha Ziara Yake Dodoma, Aelekea Jijini Mwanza Kufatilia Ajali ya MV Nyerere

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


WAZIR MKUU Kassim Majaliwa amekatisha ziara ya mkoa wa Dodoma na kuelekea Ukerewe Mwanza kuwafariji wananchi waliopatwa na maafa kutokana na ajali ya kivuko cha MV Nyerere.

Waziri Mkuu ambaye alikuwa na ziara ya kikazi ya siku saba katika mkoa wa Dodoma, ametangaza uamuzi huo leo mchana (Ijumaa, Septemba 21, 2018) wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Chandama, wilayani Chemba ambao walisimamisha msafara wake ili wamweleze kero kubwa ya maji inayowakabili.

“Nimelazimika kukatisha ziara yangu na wala sitaenda Kwa Mtoro ili niende kuwafariji wenzetu waliopatwa na msiba wa kupoteza ndugu zao kutokana na ajali iliyotokea jana usiku. Idadi ya waliopoteza maisha imefikia 91, ni msiba mkubwa kwa Taifa letu,” amesema Waziri Mkuu kwa masikitiko.

Waziri Mkuu alikuwa akitokea kijiji cha Itolwa kata ya Jangalo ambako alikuwa na mkutano wa hadhara, aliwaeleza wananchi wa vijiji vya Itolwa, Mapango na Chandama kwamba Serikali imetenga sh. bilioni 5.6 kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maji kwenye wilaya hiyo.

Akijibu kero kuhusu ubovu wa barabara, Waziri Mkuu alisema amebaini ukubwa wa tatizo la barabara hiyo yenye urefu wa km.10.3 lakini imetengewa sh. milioni 833 ambazo alisema hazitoshi.

“Mhandisi wa TARURA nenda ukakae na timu yako, inabidi mfanye upya mahesabu yenu kwa sababu barabara hii ni ndefu na ina madaraja mengi lakini pia inapita kwenye vijiji vingi. Wenzenu Kondoa wamepata sh. bilioni saba, sasa hii sh. milioni 800 hata sijui itaanzia wapi,” alisema.

“Barabara hii inapita kwenye vijiji vingi vikubwa na wakazi wa huku ni wengi. Hata kama kwa sasa hatuwezi kuijenga kwa kiwango cha lami, inapaswa ijengwe vizuri kwa kiwango kinachoweza kupitika kwa mwaka mzima,” alisema.

Aliwasisitiza watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba waache tabia ya kupenda kukaa ofisini na badala yake waende vijijini ili wakawasikilize wananchi na kutatua kero zao.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad