Bondia Hassani Mwakinyo Apata Donge Nono Sportpesa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

bondia Hassani Mwakinyo Apata Donge Nono Sportpesa
KAMPUNI ya michezo ya kubashiri ya SportPesa Tanzania, leo imefanikiwa kutoa neema ya udhamini wa miaka mitatu kwa bondia Hassani Mwakinyo.




Katika miaka hiyo mitatu Mwakinyo ataitumikia SportPesa kama Balozi wake kwenye shughuli zake zote, ambapo ataivaa nembo hiyo katika mapambano yake yote atakayofanya ndani ya miaka hiyo.


Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Harrison Mwakyembe akizungumza jambo wakati wa utambulisho huo. Kulia ni bondia Hassani Mwakinyo.



Akizungumzia kuingia kwa mkataba huo Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa SportPesa Tanzania, Tarimba Abbas, alisema wao kama kampuni wanajisikia faraja kudhamini suala la ngumi kwani imekuwa desturi yao kuhakikisha wanadhamini mambo ya michezo kwa lengo la kuwawezesha vijana kutimiza ndoto zao.


Tarimba Abbas, akishuhudia ukamilisho wa mkataba huo na Mwakinyo.

“Kudhamini vipaji kama hivi ni jambo la kawaida sasa kwetu kwani tulianza kudhamini kwenye masuala ya mpira na leo hii tunaingia rasmi kwenye ngumi, lengo likiwa ni kuhakikisha tunaimalisha michezo yote hapa nchini,” alisema.


…Akimkabidhi Mwakinyo mkataba huo.

Naye Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Harrison Mwakyembe amewapongeza Sportpesa kwa hatua hii huku akizitaka kampuni nyingine nchini kutoa udhamini katika michezo kama ilivyofanya SportPesa.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad