Saudi Arabia Kuwachunguza Wahusika wa Mauaji ya Khashoggi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Saudi Arabia kuwachunguza wahusika wa mauaji ya Khashoggi
Waziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia amesema kuwa washukiwa wote wa mauaji ya mwandishi Jamal Khashoggi, mashtaka yao yatasikilizwa nchini Saudi Arabia.

Katika kikao mjini Bahrain, Adel al-Jubeir amevishutumu vyombo vya habari vya magharibi kwa kuongeza chumvi katika kuripoti taarifa ya kesi hiyo.

Kauli yake imekuja siku moja baada ya serikali ya Uturuki kutaka kuwaamisha washukiwa 18 waliohusika na mauaji hayo.


Mchumba wa Jamal,Riyadh imekanusha madai ya kuhusishwa kwa familia ya kifalme katika mauaji hayo na badala yake imelaumu watu iliyowataja kuwa''maajenti wakatili''

Awali Saudi Arabia ilikana kuhusika kwa lolote dhidi ya mwandishi huo lakini mwendesha mashtaka wa serikali sasa ameweza kueleza jinsi mauaji hayo yalivyotokea.

Khashoggi ambaye alikuwa ni mkosoaji mkubwa wa mwana mfalme wa Saudia na viongozi wa Saudia.

Suala la kwamba washtakiwa ni raia wa Saudi ,hivyo inabidi Saudi Arabia iendelee kuchunguzwa kwa kina na washtakiwa hao watashitakiwa Saudi Arabia.

Haifahamiki kama Uturuki na Saudi Arabia wamefikia makubaliano ya kuwaamisha washitakiwa.

Hofu juu ya wapi mauaji hayo yalifanyika bado imetanda
Wasaudi Arabia wanaleza kuwa mauaji ya Khashoggi ni janga kubwa ambalo limetokea tangu shambulizi la kigaidi lililotokea mwaka 2001.
Marekani inasema kwamba bado itaendelea kuwashinikiza wasaudia kuelezea ukweli wa kifo cha mwandishi huyo kilivyotokea.

Wanasema kifo cha Khashoggi kinapaswa kuwagusa kila mmoja na hivyo Marekani haitakaa kimya kwa kitendo hiki cha kinyama alichofanyiwa mwandishi kwa vurugu.

Dakika za mwisho katika maisha ya Khashoggi kufichuliwa?
Trump amesema: "Walikuwa na wazo duni sana, na wakalitekeleza vibaya mno, na kiufupi harakati zao za kuuminya ukweli ndio mbovu zaidi katika historia ya kujaribu kuficha ukweli."

"Naamini aliyekuja na wazo lile yupo katika matatizo makubwa hivi sasa. Na wanatakiwa kuwa kwenye matatizo," amesisitiza Trump.

Nchi yeyote inayoshindwa kuzingatia sheria na kanuni za kimataifa imeshindwa.

Lakini pia rais Trump alisisitiza kuwa kuna uwezekano kuwa mfalme hafahamu mauaji hayo yalitokea vipi.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad