Sumaye Aungana Mkono Kauli ya Katibu Mkuu wa CCM

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Sumaye Aungana Mkono Kauli ya Katibu Mkuu wa CCM
Aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Fredrick Sumaye ameunga mkono kauli ya Katibu Mkuu  wa CCM, Dkt. Bashiru Ally ya kuwa vitendo vya rushwa na kutowajibika vinasababisha watu kupuuzia uchaguzi na kuuona kama ni maigizo akidai kuwa kauli hiyo ni marudio.



Akizungumza na www.eatv.tv, Sumaye amesema kuwa ni kweli watu hawana imani na kura kwakuwa amezungumza Katibu Mkuu wa chama tawala hivyo amekubaliana na vyama vya upinzani maana jambo hilo wamekuwa wakilizungumzia mara kwa mara.

Sumaye amefunguka kuwa kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2010 hadi sasa wananchi wamekuwa waoga kutokana na siasa za mihemko zilizoibuka hivi karibuni, tokea kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992.

"Uchaguzi wa mwaka 2010 ambao Bashiru aliutumia kutolea mfano niliwahi kuzungumzia kipindi hicho mara tu baadaya kutangazwa kwa matokeo, kwakuwa CCM ilipata ushindi ambao ulikuwa finyu, kwakuwa asilimia ilikuwa 25 tu ya kura zilizoandikishwa", amesema Sumaye.

Sumaye ameongeza kuwa kauli ya Dkt. Bashiru isiishie hapo akishauri chama tawala pia kufuate yale aliyosema ili kurudisha imani kwa wapiga kura.

Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally aliwahi kuzungumza kuwa vitendo vya rushwa na kutowajibika vimesababisha wananchi kupuuza uchaguzi na kuuona kama maigizo hivyo kupelekea idadi ya kura za chama chake kupungua kutokana na wapiga kura kutokuwa na imani na uchaguzi.

Dkt. Bashiru alitoa kauli hiyo Oktoba 4, 2018 mjini Morogoro katika Kongamano la Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) alipokuwa akizungumzia kuhusu umuhimu wa wananchi kuiwajibisha serikali.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad