AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mlinzi wa kushoto wa klabu ya Yanga Gadiel Michael, amerejeshwa jijini Dar es salaam kutokana na kuumia mguu kwenye mchezo dhidi ya Mwadui FC Alhamis iliyopita.
Akiongea na www.eatv.tv kocha wa Yanga Mwinyi Zahera amesema Gadiel hatakuwa sehemu ya kikosi cha Yanga kitakachocheza na Kagera Sugar kesho kwasababu imelazimika arejeshwe Dar es salaam kwaajili ya matibabu.
''Timu imefika salama hapa Kagera na tumefanya mazoezi kwa wachezaji waliopo kwenye timu isipokuwa Gadiel Michael ambaye ameumia nyama za paja hivyo imebidi arudi Dar es salaam kupata matibabu'', amesema
Zahera.
Kwa upande mwingine Zahera amesema programu yake ya mazoezi kuelekea mchezo wa Kagera Sugar inaendelea kwa wachezaji ambao hawakucheza mechi dhidi ya Mwadui kufanya mazoezi kwa saa 1:30.
Kwa wale ambao walicheza mchezo dhidi ya Mwadui FC, watafanya mazoezi mepesi. Yanga watakuwa wageni wa Kagera Sugar kesho Jumapili mchezo ambao utapigwa kuanzia saa 10:00 jioni kwenye uwanja
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK