AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Katibu wa Chadema Mkoa wa Iringa, Jackson Mnyawami amesema mkutano huo ulikuwa ufanyike leo, kwamba wamepokea barua ya polisi ikiwataka wasiendelee na mkutano huo.
Barua ya Novemba 21, 2018 iliyotolewa na mkuu wa polisi Wilaya ya Iringa kwenda kwa mbunge huyo inaeleza kuwa mkutano huo umezuiwa kutokana na taarifa za kiintelejensia.
“Polisi Iringa tunazo taarifa kuna kikundi cha watu wanaojiandaa kufanya fujo katika mkutano huo. Hali hiyo inaweza kuleta uvunjifu mkubwa wa amani,” inaeleza sehemu ya barua hiyo.
“Hakuna askari wa kutosha kwa ajili ya kusimamia mkutano huo kwani nguvu kazi kubwa imeelekezwa katika shughuli maalum za kitaifa ya usimamizi wa mitihani ya kidato cha nne, cha pili na darasa la nne.”
Mnyawani amesema wameipokea barua hiyo ya polisi ikiwa na sababu mbalimbali.
“Sababu tulizoelezwa ni za kiintelejensia kwamba kuna watu watafanya vurugu lakini pia wamesema kuwa kuna shughuli za kitaifa, ikiwa ni pamoja na mitihani inayoendelea kufanywa na wanafunzi wa kidato cha nne,” amesema.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK