Rais Magufuli amteua Pius Msekwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Rais Dkt. John Magufuli amemteua spika mstaafu, Pius Msekwa kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) na Zakia Meghji kuwa Mwenyekiti wa Braza la chuo hicho.


Rais Dkt. John Magufuli akiwa na spika mstaafu, Pius Msekwa.

Kupitia taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Gerson Msigwa imesema kuwa uteuzi huo umeanza leo Disemba 6, 2018, ambapo mbali na hao Rais Magufuli pia amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali wakiwemo wenyeviti na wakurugenzi.

"Rais amemteua Prof. Esnati Osinde Chaggu kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Samwel Gwamaka kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa NEMC", imesema taarifa.

Rais pia amemteua Meja Jenerali mstaafu Michael Isamuhyo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) na Profesa Gaspar Mhinzi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority (PURA).
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad