Video: Msigwa amjibu Askofu Kakobe, ‘Amekengeuka sana huyu mzee’

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mbunge wa Iringa Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mch. Peter Msigwa amesema kuwa kauli aliyoitoa Askofu Zachary Kakobe siku ya Jumapili katika mahubiri yake ya kuwataka viongozi wa Chadema wakatubu haiendani na heshima aliyonayo ya utumishi wa Mungu.

Ameyasema hayo jijini Dodoma alikuwa akizungumza na Dar24Media, ambapo amesema kuwa ni aibu kwa kiongozi wa dini kushangilia mapokezi ya ndege wakati watu wakipotea, wengine wakipatikana wameuawa na kupigwa risasi kwa baadhi ya viongozi.

Amesema kuwa wanapozungumzia haki za binadamu si kwasababu ya Chadema bali ni kwaajili ya Watanzania wote, hivyo anatakiwa kuelewa kuwa mabadiliko wanayoyapigania ni ya kila mmoja.

Aidha, amesema kuwa Askofu Kakobe alishawahi kutabiri mambo mengi ambayo hakuna hata moja lililowahi kutimia, hivyo amemtaka kuhubiri mambo ya haki na si ya kupendelea upande fulani ambao anaona kuna maslahi kwake.

”Ni huyu huyu Kakobe ambaye alitueleza kuwa Mrema atakuwa Rais, ni huyu huyu aliyetuambia kuwa zile nguzo za umeme pale Kanisani kwake umeme hautawaka, Ni huyu huyu anatuambia hajawahi kukutana na Lowassa wala Chadema wakati pale Mlimani City kwenye kikao cha kamati kuu alikuwepo na mimi nilimuona,”amesema Mch. Msigwa

VIDEO:
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad