Kiongozi wa upinzani Venezuela ajitangaza kuwa rais

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kiongozi wa upinzani Venezuela ajitangaza kuwa rais
Baada ya maandamano ya kumshinikiza rais Nicolas Maduro kung'atuka madarakani kukumbwa na vurugu, kiongozi mashuhuri wa upinzani Juan Guaido amejitangaza kuwa rais wa mpito.

Bw. Guaido tayari amepata uungwaji mkono kutoka mataifa ya Marekani, Canada, na majirani wa taifa hilo waliyo na ushawishi mkubwa katika kanda ya Amerika kusini kama vile Brazil, Colombia na Argentina.

Moscow imeonya kuwa hatua ya Guaido, moja kwa moja huenda ikasababisha "uvunjaji wa sheria na umwagikaji mkubwa wa damu".

Taarifa ya wizara ya mambo ya nje ilisema: "Tunaonya kuwa hatua hiyo itakuwa na athari mbaya"

Ni changamoto gani zinazomsubiri rais mpya wa DR Congo?
Huku hayo yakijiri msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa China, Hua Chunying, amesema kuwa China inapinga ''muingilio'' wa nje katika mzozo wa Venezuela.

"China inaunga mkono mikakati ya kulinda uhuru wa Venezuela wa kujitawala" alisema.

"China itaendelea kushikilia msimamo wake wa kutoingilia masuala ya ndani ya matifa mengine'."

Haki miliki ya pichaREUTERS
Image caption
Kwa mujibu wa jarida maarufu la Amerika,China iliikopesha Venezuela zaidi ya dola bilioni 62 kati ya mwaka 2005 na 2017
Uturuki, Iran, Mexico, Cuba na mataifa mengine pia yana muunga mkono Maduro.

Kwa mujibu wa msemaji wa mamlaka ya urais wa Uturuki Ibrahim Kalin, Rais Recep Tayyip Erdogan amempigia mwenzake Nicolas Maduro na kumhakikishia kuwa Uturuki itasimama nae: ''Ndugu Maduro, Simama imara, tuko nawe kwa hilo.''

Lakini hali ya taharuki inayoshuhudiwa katika ulingo wa siasa za kimataifa huenda isibadilike huku maafisa wa Marekani na Venezuela wakitupiana cheche za maneno.

Muda mfupi baada ya Rais Donald Trump kumtambua Guaido kama kiongozi wa muda wa Venezuela, Maduro alisema kuwa amekomesha mara moja uhusiano wa kidiplomasia na wa kisiasa na Marekani.
Alisema "Wafanyikazi wote wakidiplomasia na ubalozi wa Marekani nchini Venezuela" wana saa 72 hours kuondoka nchini humo.

Akijibu tamko hilo waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Mike Pompeo, amesema kuwa Marekani haitafanya mashauriano ya uhusiano kidiplomasia kupitia serikali ya Maduro isipokua Guaido.

'Watanzania, hawasubutu kuzungumza' aambiwa rais Magufuli
"Hatuoni kuwa rais wa zamani Nicolas Maduro ana mamlaka yoyote ya kisheria kuvunja uhusiano wa kidiplomasia na Marekani au uwezo wa kuwafurusha maafisa wetu kutoka nchini humo ," ilisema taarifa hiyo.

'Hatua zote za kukomesha mazozo zipo mezani'
Rais Trump aliwahi kutamka hadharani kuwa anaunga mkono "hatua ya kijeshia" nchini Venezuela mwaka 2017 na pia hakuchelea kugusia tena suala hilo katika mahojiano yake na wanahabari katika ikulu ya White House.

"Hatujafanya maamuzi lakini hatua zote za kukomesha mzozo nchini humo zipo mezani," Trump alisema.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad