AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Global Publishers wanaripoti kuwa Wawili hao wameingia kwenye mvutano baada ya kila mmoja kutoa msimamo tofauti kuhusu unasaba wa mtoto wao huyo, ambapo TID anasema ni mtoto wake, wakati mama mtu akikanusha vikali.
Kwenye mahojiano na Gazeti hilo, Shekha ambaye kwa sasa anaishi Ujerumani, alisema kuwa anachukizwa na namna TID anavyotangaza kuwa mtoto huyo ni wake, wakati siyo kweli.
Unajua huyu TID nahisi hayo madawa anayotumia (hajafafanua ni dawa za nini) yameshaanza kumuharibu, huyu mtoto sio wake kwa sababu nilishapima mpaka DNA na baba mzazi wa mtoto huyu ambaye makazi yake yapo hukohuko Bongo na majibu yakaonesha kwamba mtoto sio wa TID sasa kinachomfanya amng’ang’anie ni nini?”.
Kiukweli mimi ninachoomba TID amtoe kabisa huyu mtoto akilini mwake, kwa sababu kwanza mwanangu hajui hata kama ana baba anaitwa TID na tulishaondoka huko Tanzania tangu binti yangu akiwa na umri wa mwaka mmoja na miezi kumi… na sasa ana miaka mitatu, atakuwa ameshamsahau kabisa.”
Kwa upande wa TID alifunguka na kusema kuwa anachokifahamu na hakitabadilika akilini mwake ni kwamba Tania ni mtoto wake.
Huyu mwanamke ananishangaza sana, kwa sababu mimi ninachojua huyo mtoto ni wangu na mpaka kuondoka kwake hapa mimi ndio nilikwenda ubalozi kusaini ndio mtoto akapata Visa ya kusafiri.
Sasa simuelewi anavyosema nikae mbali na yule mtoto, isitoshe mimi nina mpaka ushahidi wa vyeti. Tania ni mwanangu na atabaki kuwa mwanangu siku zote”.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
USHAHIDI WA VYETI HAUTOSHI PIMA DNA wewe
ReplyDelete