AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola ameagiza mkurugenzi wa kampuni ya wawekezaji kutoka falme ya Kiarabu ya Ortello Business Cooperation(OBC), Isack Mollel kukamatwa kwa tuhuma za kuwaingiza nchini wafanyakazi wa kigeni bila kufuata taratibu.
Lugola ametoa agizo hilo leo Jumatano Februari 13, 2019 katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Arusha.
Amemuagiza kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Longinus Ribishumbwamu kumsaka mkurugenzi huyo kabla hajamaliza ziara yake jijini Arusha.
Amesema mkurugenzi huyo alitakiwa kujisalimisha polisi tangu wiki iliyopita sambamba na wafanyakazi 10 wa kampuni hiyo, waliokuwa wameingia nchini kinyume cha sheria ambao tayari wamefikishwa mahakamani na kesi yao itatajwa tena Februari 22, 2019.
"Kazi ambazo walikuja kufanya wafanyakazi hao zinaweza kufanywa na Watanzania hivyo kisheria hawakupaswa kuja nchini kufanya bila kufuata utaratibu,” amesema.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK