AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mbowe ametoa shukrani hizo baada ya kukaa rumande kwa zaidi ya miezi mitatu baada ya kudaiwa kukiuka masharti ya dhamana yeye pamoja na Mbuge wa Tarime Mjini Esther.
Katika ujumbe huo, Mbowe ameanza kwa kusema, “Naomba niwashukuru sana wale wote walioshiriki nasi kupigana, kulia na hata kuimarishana kwa njia mbalimbali katika kipindi chote cha miezi mitatu na nusu tuliyoishi gerezani.”
“Natambua na kuheshimu mno ushiriki wenu kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na sala, ushauri, huduma ya chakula, michango ya fedha, solidarity support mahakamani na zaidi walioweza kutenga muda wao na kuja kututembelea na kutufariji gerezani Segerea kulikoambatana na zawadi mbalimbali vikiwemo vitabu na magazeti, matunda, maji, juisi na hata machozi!!!.
“Nitambue kipekee kazi kubwa na ya kutukuka iliyofanywa na Mawakili Wasomi waliounda defence team yetu!! You were great all the way through!!
"Nitoe shukrani vilevile kwa wale wote waliotoa support kwa familia zetu na hata kututunzia na kujenga kwa njia mbalimbali majimbo yetu ya uchaguzi ikiwemo kazi ya Chadema ni Msingi.”
“Kwa wale walioshindwa vyote hivyo, watambue kwa dhati nawapenda na kuwaombea yote yaliyo mema... au kama wapo wengine waliokwazika kwa njia moja au nyingine.... pia nichukue fursa hii kuwaomba msamaha na kuitaka amani miongoni mwetu!!.
"Niwape pole nyingi wenzetu wote waliokumbwa na masahibu mbalimbali katika kipindi chote hiki!! Tuimarishwe zaidi katika mapito haya ili itimie kauli ya “kesho yetu kuwa bora kuliko jana.Mbarikiwe sana!!" Amesema Mbowe
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK