TAKUKURU Yaomba Kumhoji Jamal Malinz

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), imeiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa mara ya pili, kumhoji aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Jamal Malinzi na Katibu wake, Selestine Mwesigwa.

Ombi hilo limewasilishwa mahakamani hapo na Wakili wa Serikali wa TAKUKURU, Leornad Swai mbele ya Hakimu Mkazi, Maira Kasonde, baada ya shahidi wa 11 katika kesi hiyo kumaliza kutoa ushahidi wake.

Swai amedai kuwa Januari 16, 2019 waliomba kuwahoji washtakiwa hao, lakini hawakuweza kwa sababu walitoa sababu zao kuwa wahojiwe siku nyingine.

“Tunaomba tena kwenda kuwahoji washtakiwa, kwa sababu tayari Mahakama ilishatoa oda hiyo Januari 16, mwaka huu” Swai

Baada ya Swai kumaliza kuwasilisha, Hakimu Kasonde alikubaliana na ombi hilo na kutoa ruhusa kwa TAKUKURU kuwachukua kwa ajili ya mahojiano

Hakimu Kasonde alisema washtakiwa hao watahojiwa Machi 8, 2019 na kesi itaendelea kusikilizwa Machi 19,2019.

Mbali ya Malinzi na Mwesigwa, mshtakiwa mwingine ni Mhasibu wa shirikisho hilo, Nsiande Mwanga, Meneja wa ofisi ya TFF, Miriam Zayumba na Karani Flora Rauya, ambapo wanakabiliwa na mashtaka 28 yakiwemo ya utakatishaji fedha ambazo ni USD, 375,418.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad