AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Tukio hili linakuja takribani miongo miwili baada ya mtoto mwengine kuzaliwa katika mazingira kama hayo. Mtoto huyo, Rosita Mabuiango alizaliwa wakati wa mafuriko yaliyokumba maeneo ya kusini mwa Msumbiji.
“Nilikuwa nyumbani na mwanangu wa kiume mwenye umri wa miaka miwili ambapo ghafla , bila onyo lolote, maji yalipoanza kuingia ndani ya nyumba yetu,” Amélia aliliambia shirika la watoto la Umoja wa Mataifa Unicef.
“Sikuwa na njia nyingine ila kukwea mti, nilikuwa peke yangu na mtoto wangu wa kiume.”
Amélia na familia yake kwa sasa wanaishi katika makazi ya muda ya msaada karibu na Dombe, na wanaarifiwa kuwa katika afya nzuri.
Rosita Mabuiango, ambaye sasa ana umri wa miaka 19, aligonga vichwa vya habari za kimataifa baada ya yeye na mama yake Sofia kuokolewa na helikopta kutoka kwenye mti uliokuwa umezingirwa na maji ya mafuriko.i
Akizungumza na magazeti nchini humo Mail na Guardian, Sofia alisema kuwa alikuwa na uchungu “mkali , mkali sana.”
“Nilikuwa najaribu kulia , kupiga mayowe. Wakati mwingine nilifikiri mtoto alikuwa anatoka, lakini wakati mwingine nikafikiri ilikuwa ni kwa sababu ya njaa .”
Aliongeza kusema kuwa : “Watu wengi walipoteza kila kitu katika mafuriko, lakini walau nilipata kitu .”
Rosita Mabuiangoakizungumza na BBC
Image captionRosita Mabuiango pia alizaliwa juu ya mti wakati mafuriko yalipopiga eneo la kusini mwa Mshumbiji mwaka 2000
Lakini katika mazungumzo na BBC, Rosita alisema kuwa ahadi za serikali ya Msumbiji za kumlipia masomo, na ahadi ya kumlipia gharama ya safari ya Marekani iliyotolewa na serikali ya Marekani zote hazijatimizwa.
“Masomo yangu yamekuwa wakati wote yakigaramiwa na mama yangu, sijapokea chochote kutoka kwa serikali ,” alisema Rosita.
Maporomoko ya rundo la takataka yaua watu 17 Msumbiji
“Sawa , nyumba tulijengewa na serikali lakini kwa sasa haiko katika hali nzuri. Mvua inaponyesha, nyumba inavuja. Walau wangesaidia kuikarabati .”
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK