AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kufuatia hatua hiyo Kamati imetoa mapendekezo ya Bunge kutofanya kazi na CAG,Prof.Asaad.
Akisoma ripoti ya kamati hiyo bungeni leo Aprili 2 mwaka 2019, mwenyekiti wa kamati hiyo, Emmanuel Mwakasaka amesema kamati yake imemtia hatia kwa kuvunja kifungu cha 26 E cha Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge.
Amesema Profesa Assad wakati wa mahojiano na kamati hiyo alionyesha dharau na hakuonyesha kujutia maneno yake
"Prof. Assad alikiri mbele ya kamati kuliita Bunge dhaifu lakini alipingana na tafsiri ya neno 'dhaifu' iliyopo kwenye Kamusi ya Kiswahili Sanifu inayosema 'goigoi, hafifu, isiyo imara' akisitiza kiuhasibu udhaifu ni 'upungufu'.
"Tuliangalia maana ya neno upungufu kwenye kamusi tukabaini ni 'isiyo kamili, isiyo imara', hivyo alidhamiria kulidhalilisha Bunge.
"Tulimuuliza CAG Assad kama ataacha kulitumia neno udhaifu akasisitiza ataendelea kulitumia na hakujutia kulitumia dhidi ya Bunge.CAG hakuomba msamaha wala kujutia na akasisitiza ataendelea kulitumia neno hilo".Amesema Mwakasaka
Baada ya ripoti hiyo ya kamati, Naibu Spika, Dk Tulia Ackson alitoa nafasi kwa wabunge kujadili jambo hilo huku wabunge wakipishana maoni yao, kukubaliana na uamuzi huo na wengine kupinga .
Baada ya wabunge kutoa maoni yao, Dk Tulia amelihoji Bunge kuhusu hoja hiyo, akiwakata wanaokubaliana na jambo hilo kusema ndio na wasiokubaliana na suala hilo kusema sio, "waliosema ndio wameshinda. "
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK