CUF Wamshitaki Zitto Kabwe na Maalim Seif Mahakamani.....Wanadai Fidia ya Milioni 900

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Chama cha Wananchi CUF  kumemfungulia kesi mbili katibu wake mkuu wa zamani, Maalim Seif Sharif Hamad na wenzake, kikiwadai fidia ya jumla ya Sh900 milioni.


Kesi hizo zimefunguliwa na Bodi ya Wadhamini CUF katika Mahakama Kuu Zanzibar na Mahakama Kuu ya Tanzania dhidi ya Maalim Seif na wenzake akiwamo Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, kikiwadai fidia hiyo kutokana na uharibifu uliofanywa katika ofisi zake.


Katika kesi hizo, chama hicho kinadai kuwa uharibifu huo ulifanywa na mawakala au wawakilishi wa Maalim Seif na wenzake muda mfupi tu baada ya kutangaza kujiunga na ACT-Wazalendo.


Maalim Seif alijiunga ACT-Wazalendo Machi 18 muda mfupi baada ya uamuzi wa Mahakama Kuu uliomhalalisha Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mwenyekiti halali wa CUF) na siku chache baada ya Baraza Kuu la Uongozi la CUF kutangaza kumvua uanachama yeye na wenzake.


CUF inadai kuwa kufuatia uamuzi huo, Maalim Seif, Zitto na wenzao kwa msaada wa mawakala na au wawakilishi wao, walipaka rangi ya chama cha ACT-Wazalendo katika majengo mbalimbali ya ofisi za CUF, ngazi ya matawi na wilaya Zanzibar na Bara.


Kwa mujibu wa hati za madai, chama hicho kinadai kuwa mawakala na wawakilishi hao wa Maalim Seif na wenzake walifanya uharibifu huo kwa ushauri wa mmoja wa wadaiwa katika kesi hizo, Daimu Halfan, huku wakijua kuwa ni kinyume cha sheria


Uharibifu mwingine unaodaiwa ni kushusha na kuchoma bendera zake na kisha kupandisha za ACT- Wazalendo katika ofisi zake, kuondoa na kuharibu samani na nyaraka za ofisini.


Chama hicho kinapinga madai ya baadhi ya wadaiwa (Mazrui, Faki na Juma) kwamba majengo hayo yalikuwa ni ya watu binafsi waliokuwa wameyatoa kwa chama hicho kumuunga mkono Maalim.


Badala yake, CUF inadai kuwa tangu mwaka 1992, kimekuwa kikimiliki majengo kilipoanzisha ofisi zake katika ngazi za matawi na vijiwe, ambayo kiliyanunua maeneo ya Mabibo na Magomeni Dar es Salaam, Tanga mjini na maeneo mengine Tanzania Bara.


Katika kesi namba 60 iliyofunguliwa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, wadaiwa ni Zitto (mdaiwa wa kwanza), Maalim Seif (mdaiwa wa pili) na wenzao saba.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad