Mahakama ya Juu ya Uganda Yamsafishia Njia Museveni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mahakama ya juu ya Uganda yamsafishia njia Museveni
Mahakama ya Juu nchini Uganda imekubaliana na uamuzi wa kuondosha ukomo wa umri wa mgombea urais, na hivyo kumsafishia njia Rais Yoweri Museveni mwenye umri wa miaka 74 kuwania kwa muhula mwengine wa sita. 

Mahakama hiyo ilitupilia mbali zuio la wapinzani, ambao waliukatia rufaa uamuzi wa mahakama ya katiba ulioridhia mabadiliko ya katiba yaliyofanywa na bunge. 

Katika uamuzi wake hapo jana, Jaji Mkuu Bart Katureebe alitangaza kwamba rufaa hiyo imeshindwa, baada ya majaji wanne kuitupilia mbali dhidi ya watatu walioiunga mkono.

Mwezi Disemba 2017, Rais Museveni - ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 1986 - aliusaini muswaada wa sheria kuondosha ukomo wa umri kwa wagombea urais, na hivyo kuashiria kuwa angeliwania tena mwaka 2021. 

Uamuzi huo ulizusha ukosoaji mkubwa kutoka kwa wapinzani, ambao wanamtuhumu kiongozi huyo kutaka kuwa rais wa maisha.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad